Thursday, 16 February 2017

DALILI ZA UTI

            Dalili Za Uti

UTI, yaani Urinary Tract Infections, ni magonjwa au maambukizi katika njia ya mkojo. Maambukizi hayo huletewa na vimelea (bakteria) au kitu chochote kinachoweza kusababisha shida katika njia ya mkojo.
Vitu hivi vinaweza kuingia kwenye njia ya mkojo kutoka nje au ndani ya mwili. Maambukizi haya hayabagui jinsia wala umri, kwani yanaweza kumpata yeyote.
Dalili Za Uti
UTI usipotibiwa, unaweza kuenea na kuadhiri viungo vingine vinavyoshikana na njia hii kama vile kibofu cha mkojo (bladder), mirija inayoshikanisha kibofu cha mkojo na figo (ureter) na sehemu inayotoa mkojo kutoka kwenye kibofu na kuutoa nje (urethra). Kwa ufupi, UTI huadhiri viungo ambavyo hupitisha mkojo kutoka mwilini na kuutupa nje.
Wanawake huadhirika zaidi na UTI ikilinganishwa na wanaume. Hii ni kwasababu za kimaumbile. Maambukizi haya huweza kusababishwa na historia ya familia au kufanya mapenzi na watu kadhaa bila kutumia kinga.
Wasichana wadogo walio chini ya umri wa miaka miwili na wavulana ambao hawajatahiriwa pia huupata ugonjwa huu mara zaidi.
Vimelea vinavyosababisha UTI ni kama vile Staphylococcus saprophyticus na Escherichia coli (E Coli). Asimilia chache ya maambukizi haya huweza kuletwa na virusi au fangasi (fungus).

Dalili za UTI

Dalili za UTI ambazo mtu hupata hulingana na sehemu ambayo imeathirika. Hivyo basi, dalili zitakua tofauti wakati mrija wa mkojo, kibofu au figo zimeathirika. Dalili hizo zimeelezwa kwa kina hapa.

Dalili iwapo mrija wa kutoa mkojo kwenye kibofu umeathirika

  • Mtu huhisi kama kwamba anachomeka wakati anapokojoa. Kuchomeka huko huweza kuzidi na kuwa uchungu (maumivu).
  • Shida wakati wa kukojoa kama vile kushindwa kudhibiti kasi ya mkojo.
  • Mtu anaweza kukawia sana kabla ya mkojo kutoka.
  • Mtu kuhisi kukazwa sana lakini aendapo chooni, mkojo kidogo tu ndio hutoka.
  • Kukojoa kiasi kidogo cha mkojo mara nyingi.

Dalili za UTI iwapo kibofu cha mkojo kimeathirika

  • Mtu huweza kuona damu kwenye mkojo anapoenda haja. Hii huweza ikawa dalili ya UTi ingawaje magonjwa mengine pia huleta dalili sawa na hii.
  • Pia mtu huweza kuhisi maumivu kwenye nyonga (hip area). Hii huathiri wanawake zaidi.
  • Kuhisi kama kibofu kimejaa wakati wote.
  • Dalili ingine ni kuwa na maumivu chini ya kitovu.
  • Dalili ya mwisho ni mtu kukujoa mara kwa mara na kuhisi uchungu anapokojoa.

Dalili iwapo figo zimeathirika

  • Mtu hupata kichefuchefu mara kwa mara iwapo ugonjwa wa UTI umemwathiri. Kichefuchefu ni hali ya kuhisi kutapika.
  • Maumivu kwenye mbavu.
  • Dalili hii ya kichefuchefu huweza kuzidi na mwathiriwa kuanza kutapika anapokula chakula.
  • Dalili ingine ni mtu kuumwa na upande wa juu wa mgongo. Hii inaweza kuwa kuanzia katikati ua uti wa mgongo, kwenye mabega na kwenye shingo.
  • Dalili hizi huweza kuambatana na homa kali.
  • Dalili ya mwisho ni mtu kuhisi baridi kali na kutetemeka sana pasi na kuwepo kwa baridi.
Kuna dalili za UTI  ambazo hutokea wakati ugonjwa huu umeathiri mahali popote kwenye njia hii ya kutoa mkojo. Nazo ni kama rangi ya mkojo kugeuka na kuwa mawingu mawingu, pia unaweza ukawa rangi ya brauni au pinki.
Maradhi yanapozidi, mkojo huwa na rangi nyekundu na wenye harufu kali. Wanaume huweza kupata maumivu wakati wa kwenda haja kubwa.

Hatari za UTI

Magonjwa yanayosababisha UTI ni rahisi kutibiwa kutumia dawa za antibaotiki. Hata hivyo, mtu huhimizwa kupata matibabu mara moja na kumaliza dawa kama alivyoagizwa na daktari. Maradhi haya yasipotibiwa huweza kuleta shida zaidi kama vile:
  • Maradhi kujirudia baada ya kutibiwa na kupona kabisa. Hii hutokea sana sana kwa wanawake ambao wanaathirika na UTI zaidi ya mara tatu.
  • Kuharibika kwa figo kutokana na shida zinazotokea kama vile kidney infection (Pyelonephritis). Hii huweza kutokea mtu asipopokea matibabu.
  • Wanawake huweza kuwazaa watoto mapema (premature birth) au kuzaa watoto wenye uzani mdogo zaidi.
  • Njia ya mkojo (urethra) kwa wanaume hufinyika na kuwa ndogo. Hii hutokana na ugonjwa wa Urethritis kutokea mara kadhaa. Pia maradhi kama gonococcal urethritis huweza kusababisha shida hii.
  • Mwisho, ugonjwa wa UTI unapofika kwenye figo kupitia mshipa wa kutolea mkojo, mtu huweza kupata Sepsis. Hii ni shida inayokumba figo na kuziangamiza kabisa. Hii ni mojawapo ya shida hatari kabisa kwani inaweza kumfanya mwathiriwa kuaga.

Hali zinazochangia kupata maradhi ya UTI

  • Maumbile: Wanawake huwa na njia fupi ya kutoa mkojo (urethra) kuliko wanaume. Hivyo basi, vimelea na vitu vinavyosababisha UTI huweza kuingia kwenye njia ya mkojo haraka.
  • Ngono: Watu wanaofanya mapenzi huambukizwa UTI zaidi ya wasiofanya mapenzi kama vile watoto. Walio na wapenzi wengi huwa hatarini ya maambukizi zaidi.
  • Njia za kupanga uzazi: Wanawake wanotumia njia za diaphragm kupanga uzazi hupata maambukizi zaidi ya wanaotumia kinga aina ya spermicidals.
  • Kufunga uzazi: Wanawake waliofikisha miaka ya kufunga uzazi huwa hatarini zaidi kutokana na upungufu wa estrogen.
  • Kukosa kinga mwilini: Mtu anapokua na maradhi yanayopunguza kinga ya mwili kama vile ugonjwa wa sukari au Ukimwi, anaweza kuupata ugonjwa huu kwa urahisi.
  • Upasuaji: Iwapo mtu amefanyiwa upasuaji karibu na njia ya mkojo, inaongeza uwezekano wake wa kupata UTI.
  • Kufungika kwa mishipa ya figo: Mawe yanayokuwa kwenye figo huleta shida za kufungika kwa mishipa ya kutoa mkojo kwenye figo. Hii huweza kuongeza uwezekano wa maradhi ya UTI.
  • Shida za njia ya mkojo: Watoto wengine huzaliwa wakiwa na shida kwenye njia zao za mkojo. Kwa mfano hawawezi kudhibiti mkojo au wanatumia vifaa vinavyowasaidia kutupa mkojo nje. Hii ni njia inayoongeza hatari ya kupata UTI.

Matibabu

UTI hutibiwa kwa dawa za antibaotiki. Hata hivyo vimelea vya UTI huweza kuzoea dawa na kutopona. Hii hutokea sana sana mtu anapopata ugonjwa huu zaidi ya mara tatu kwa mwaka.
Hii inapofanyika, daktari huweza kumpangia mtu njia spesheli za kupambana na UTI. Njia hizo za matibabu ni:
  • Kunywa dawa za antibaotiki kwa kiasi kidogo kwa muda mrefu. Hii huzuia kuchipuka tena kwa maradhi ya UTI.
  • Kunywa dosi moja ya antibaotiki mara tu mtu anapofanya mapenzi. Ngono ni njia inayoongeza kutokea kwa maradhi haya.
  • Kunywa antibaotiki kwa siku moja au mbili dalili zinapoanza kujitokeza.
  • Kutumia bidhaa za kujipima nyumbani na kujua iwapo maradhi yamo au yanaanza kutokea

Hitimisho

Dalili  za UTI ambazo zimetajwa hapa ni baadhi ya zile ambazo huhusishwa sana na maradhi ya UTI. Hata hivyo, ugonjwa huu ni mgumu kujua iwapo upo bila kupimwa na daktari.
Hivyo basi, maandishi haya yanafaa kusaidia mtu kuuelewa ugonjwa wa UTI tu. Mtu anapoona kuwa ana dalili hizi, anahimizwa kufika kituoni cha afya ili kutibiwa mapema.

Utafiti

  1. http://www.webmd.com/women/guide/your-guide-urinary-tract-infections?page=2
  2. http://www.mayoclinic.org/diseases-conditions/urinary-tract-infection/basics/risk-factors/con-20037892
  3. http://www.nhs.uk/Conditions/Urinary-tract-infection-adults/Pages/Introduction.aspx
  4. http://www.nhs.uk/Conditions/Urinary-tract-infection-adults/Pages/Introduction.aspx
  5. http://www.healthline.com/health/bladder-infection
  6. http://www.medicinenet.com/urinary_tract_infection/article.htm
Publicado el

Deja un comentario

Tu dirección de correo electrónico no será publicada. Los campos obligatorios están marcados con *




MESSAGE ZA MAPENZI



     Message za      Mapenzi

Kupendwa au kependana ni jambo ambalo limekubalika katika jamii. Mapenzi kati ya wapendanao hujengwa kwa maneno matamu ya kuufurahisha mtima wa mchumba wako au yeyote youle unayemtumia arafa za mapenzi.
Kwa arafa nzuri za mapenzi zitakazomsisimua na kumburudisha mpenzi wako, soma makala haya hadi mwisho.
Message za mapenzi
  1. Naweza kukupa masikio yangu usikilizie, mabega yangu ulalie, miguu yangu utembelee na mikono yangu ushikie. Kitu kimoja  siwezi kukupa ni moyo wangu kwani tayari nilishakupa zamani.
  2. Nimezihifadhi hisia zako katika moyo wangu. Nakuahidi kuwa sitawahi punguza upendo wangu kwako. Kwa hivyo, tunza arafa hii ya ahadi kwenye simu yako, ili iwe kumbukumbu kila uisomapo! “nakupenda sana malaika wangu.”
  3. Wewe ni wapekee na ninakupenda sana. Sifikirii kukusaliti na wala sina wazo la kukutenda mambaya. Nakuomba tuendelee kupendana siku zote Mpenzi wangu.
  4. Nashtakiwa kwa kumpenda msichana fulani aliyeutesa sana moyo wangu. Mahakama imenihukumu kifo na kifaa kitakachoninyonga ni upendo. Lakini Raisi Mapenzi amenisamehe na akaamrisha nimehukumiwe kuwa mwaminifu kwa mschana huyo na kumpenda milele. Nakupenda mpenzi wangu.
  5. Natamani niwemachozi machoni mwako ambapo ningeteremka na kuishia midomoni mwako. Lakini sitamani kamwe uwe machozi machoni mwangu. Maana nitakupoteza kila muda niliapo.
  6. Aha! Cjui ni kwa nini nina hamu ya kulifaidi penzi lako kiasi hiki? Natamani uwe karibu nami unipime ugonjwa huu na pia unitibu. Kwani wewe ndiye daktari wa kipekee ninaye mwamini kwa moyo wangu wote. Nahisi nazidi kuchanganyikiwa kwa kukosa penzi lako.
  7. Thamani ya penzi lako ni kubwa kwangu, siwezi kuifananisha na chochote katika ulimengu. Kwa hivyo sina budi kumshukuru muumba, kwa kunipa mpenzi mwema anayezijali hisia zangu na kunipenda kwa dhati. Usiache kunipendampenzi wangu.
  8. Kila tunapokuwa chumbani nawe mpenzi wangu, huwa natamani niwe mbunifu na pia huwa najitahidi kuepuka udhaifu ili penzi langu kwako lisikukifu. Kwa hivyo, endelea kulifurahia peni langu mpenzi.
  9. Mapenzi yana raha na ni matamu pia. Hamu ya kuwa nawe hainiishi kwa sababu siku zote wanipa raha. Umuhimu wako kwangu haufananishwi na chochote duniani. Moyoni mwangu unang’aa kama nyota ya jaha. Nakusihi ulitunze penzi letu mpenzi wangu.
  10. Moyo wangu unadhamiria kukupenda wewe pekee. Kupenda kwa dhati siku zote bila pigamizi lolote lile. Kwa hivyo, nipende nami nitakupenda na tudumishe mapenzi ya dhati.
  11. Niruhusu nitamke neno ambalo halina gharama na hutumiwa vibaya na kwa wengi halina thamani wala maana. Siwezi kuliandika neno hili kwa karatasi wala kulitamka neno hili pasi na kukumbuka uso wako. Ningependa kukujulisha ya kwamba neno hili hutufanya mimi na wewe tuwe pamoja japo tuko kusi na kasi. “ Nupenda mpenzi wangu.”
  12. Uliwahi kufikiria upendo ni nini? Upendo ni jawabu kuwa kila mmoja anataka… kwa hivyo, upendo ni lugha. Mimi na wewe tunaongea, lakini hatuwezi kuununua upendo. Upendo ni kama uchawi safi na ndiyo siri kuu ya maisha mazuri. Nakupenda Mpenzi.
  13. Zidhamirii kuukabidhi mtima wangu kwa mwingine ila wewe. Nataka uelewe kuwa wewe ni wa kipekee maishani mwangu. Nipende mpenzi na nahaidi kuwa nitalienzi penzi lako daima.
  14. Mapenzi ni kama utoto, deka ulie na tikumbebeleza mpenzi wangu. Penzi ni kama zawadi, tabasamu na ulibusu shavu langu halafu uniambie kiasi gani wanipenda. Lakini, jua kuwa jina lako limeandikwa katika moyo wangu kwa wino usiofutika.
  15. Nimezuguka sana nikiyaangaza macho angalau nipate mschina mrembo wa kumpa moyo wangu, moyo uliojaa upendo, alile tunda lililomo huku nikimpa mahaba ya dhati. Kwa bahati nzuri, uliuteka moyo wangu na nishaukabidhi kwako. Tulitunze penzi mpenzi wangu.
  16. Je, unakubali au unakana kwa mujibu wa sheria za mahakama ya mapenzi kifungu cha mahaba unahukumiwa kunipenda siku zote? Utakubali kukata rufaa kwa sababu hujatendewa haki?
  17. Wengi husema mapenzi ni upepe, mimi sivumi na kupotea. Pia wakasema kuwa mapenzi ni mahaba, mimi sili nakamaliza. Wakamalizia na kusema kuwa mapenzi ni raha, na mimi siwezi kuipeza. Nipenda nami nikupende, tupendane tufunzane utamu wa mapenzi.
  18. Japo mbinguni sijafika, lakini najua vizuri mtoto umeumbika kama malaika. Nina uhakika kwamba kila mwanamume akikuona hana budi kutokwa na udenda. Naomba uniruhusu nikueleze ninavyohisi moyoni mwangu kwani nimeshindwa kuficha kukueleza jinsi ninavyokupenda. Amini ninakupenda sana.
  19. Najua kuwa utarejea nyumbani ukiwa umechoka. Tafadhali badilimavazi yako, halafu uingie bafuni kujimwagia maji. Nitamani nikusaidie kuusugua mgongo wako na pia nikuandalie chakula, lakini siku haijawadia mpenzi.
  20. Mapenzi yanalewesha ingawa si pombe, yanapoesha ingawa si dawa. Mpenzi humfanya mtu alie na ingawa si katuni, inkufanya uchecke. Ni mimi tu mwenye mapenzi ya dhati kwa, nipende nami nikupende, tupendane siku zote.
  21. Weupe wa mapenzi yako kwangu ni kama mwezi angani. Mahaba na ucheshi wako siwezi kufananisha na chochote. Ninaposema kupata mfano wako hautawahi kutokea, niamini. Elewa kuwa nakupenda na sikuachi asilani.
  22. Sijui nikueleze vipi ili uelewa kuwa moyo wangu umejaa penzi lako. Kila nifikiriapo mbona una walakini na huniamini ninaposema kuwa ni wewe pekee ninayekupa mahaba yangu. Tafadhali mpenzi, rudisha imani yako na uamini ni wewe ninayependa pekee duniani.
  23. Kwa kawaida, busu la amani hubusiwa kwa mashavu, busu la mafanikio usoni, busu la upendo ndomoni, na busu la mapenzi shingoni. Je, ungependa nikupe busu gani mpenzi?
  24. Mpenzi, elewa kuwa ni wewe sababu ya huu usingizi. Najilaza kitandani nikiamini kuwa tutakutana kwenye njozi, njozi ya kuyaenzi mapenzi yetu. Nakupenda sana.
  25. Najua umechoka sana hata akili yako. Huu ndio wakati wako wa kupumzika na ninakutakia usiku mwanana. Lakini wacha moyo wako uwe macho ya kumuona anayekupenda kwa dhati. Pokea busu mpenzi wangu.
  26. Natamani sana kuyaona macho yako yakifumbua, pia nataka kuzisikia sauti zako za ndoto zako. Natamani zaidi kukuona ukijigeuza kitandani. Nikukumbuka busu lako la kunitakia usiku mwema, nakutamani wewe.
  27. Mpenzi, najua wanaokutamani ni wengi lakini elewa kwamba ni mimi tu kati yao mwenye mapenzi ya dhati. Ziba masikio usiwasikie kamwe, nia yao ni kutugombanisha. Nipende daima mpenzi wangu.
  28. Utamu wa samaki ni kula na wali, na usikimbie nyuki ukakosa asali. Ni mimi tu niliyeshughulika kukujulia hali. Umeshinda aje sakafu ya moyo wangu?
  29. Furaha yangu ni kuwa nawe kwani u zaidi ya mboni yangu. Najisifu kuwa nawe maishani mwangu na ninaamini siku itatokea ilikuwa karibu nawe mpenzi wangu, unisahaulishe machungu na karaha za huu ulimwengu.
Tumia arafa hizi za mapenzi zitakuwezesha kuufurahisha moyo wa umependaye.
Publicado 

Deja un comentario

Tu dirección de correo electrónico no será publicada. Los campos obligatorios están marcados con *




MISEMO YA KISWAHILI

60 Misemo ya Kiswahili

Misemo ni kauli fupifupi ambazo hutumiwa na jamii kusisitiza ukweli wa jambo fulani. Kauli hizi huunganisha mawazo au dhana tofauti kuwa mwili mmoja na kupitisha ujumbe uliodhamiriwa na mnenaji au mwaandishi.
Pia, misemo ni fungu la maneno ambalo hutumiwa na jamii tofautitofauti kwa lengo la kusisitiza maadili fulani.
Misemo ya Kiswahili
Kwa mfano tukisema mtu amegonga mwamba hatumaanishi kwamba amepiga jiwe kubwa kwa kifaa chochote au kwa mkono, bali tunamaanisha kwamba ameshindwa kuendelea katika jambo fulani.
Ifuatayo ni misemo ya kiswahili na maana yake.
  1. Kupata jiko
Huu msemo haumaanishi kununua au kuazimz jiko la kupikia. Una maana ya kupata mke au kuoa. Kwa hivyo, mtu anaposema nimepata jiko anamaanisha kuwa ameoa.
  1. Kuangusha uso
Maana ya huu msemo ni kuona aibu au soni mbele ya watu kwa jambo mbaya ulilolitenda. Mfano wa matumizi ni kama: ukitenda mema hapatatokea haja ya kujishusha hadhi kwa kuangusha uso kila wakati.
  1. kuenda mbwehu
Maana yake ni kutoa hewa mdomoni. Naneno lingine lililo na maana sawa na kuenda mbwehu ni kuteuka. Mfano wa matumizi ya msemo huu ni kama vile: Kwenda mbwehu ugenini ni dalili ya ulafi.
  1. Enda msobemsobe
Maana kamili ya msemo huu ni kuenda pasipo na utaratibu wowote. Pia huweza kumaanisha kuenda pasipo na hiari. Mfano katika sentensi: alipougua malaria alikuwa akienda msobemsobe.
  1. Enda mvange
Kabla ya kutoa maana ya msemo huu, ni vizuri uelewe kuwa maana ya neno ‘mvange’ ni ‘kombo’. Kwa hivyo mesomo huu unaweza kuwa ‘enda kombo,’ na maana yake mambo kufanyika kwa namna isiyotarajiwa. Kwa mfano, namshukuru Mola kwa sababu biashara yangu haikuenda mvange.
  1. chokoza nyuki mzingani
Mzinga ni nyumba ya nyuki. Musemo huu unamaanisha kuenda palipo na hatari na kujaribu kuichokoza au kuikabili kijiga hatari hiyo. Mfano katika sentensi: kung’oa simba usinga wake wa shingoni ni mfano wa kumchokoza nyuki mzingani.
  1. Bwaga wimbo
Maana yake ni kuanzisha au kuongoza wimbo. Msemo huu huwezeka kutumika katika sentinsi kama ifuatayao; mahadhi ya aliyeubwaga wimbo yalikuwa mazuri.
  1. Anua majamvi
maana ya msemo huu ni kutamatisha jambo au shughuli fulani uliyoanzisha. Pia kukunja jamvi ina maana sawa na kuanua majamvi. Kwa mfano, baada ya wanariadha kuanua majamvi yao, walirejea nchini.
  1. Choma mkuki
Maana ya msemo huu ni ‘kufuma’ au ‘shambulia’ kwa kutumia mkuki. Kwa mfano, siku hizi vituko ni vyingi, aghalabu watoto wanawachoma mikuku wenzao kwa utesi wa mashamba.
  1. Fanya ndaro
Neno ndaro linamaanisha sifa au sifu. Msemo huu unamaashisha kujisifu kwa jinsi mtu anavyozumgumza. Kwa mfanfo, ni vizuri uyaeleze yote uliyoyapitia bila ya kujifanyia ndaro na kumbe hamna lolote.
  1. Fanya speksheni
Speksheni ni neno ambalo lina maana sawa na ukaguzi. Hivyo basi, msemo huu unamaanisha fanya ukaguzi au kagua. Kwa mfano, mkubwa wa kituo cha polisi hufanya speksheni ya nyumba zote za polisi kila jumapili.
  1. Fanya udhia
Msemo huu unamaanisha kufanya usumbufu. Kwa mfano, hakudhamiria kufanya udhia kwa matamshi yake kwani aliyoyasema ni ya kweli.
  1. Arusi ya mzofafa
Neno ‘mzofafa’ lina maana sawa na maringo au madaha. Arusi ya mzofafa ina maana sawa na arusi iliyonoga kwa mbwembwe na hoihoi. Kwa mfano, Bwana alituandalia arusi ya mzofafa hatutaisahau.
  1. Kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa
Msemo huu una maana kuwa unapewa sifa usizostahili. Msemo mwingine ulio na maana sawa ni kuvalishwa kilemba cha ukoka.
  1. Chezea unyango wa kima
Msemo huu huweza kutumika kuonya mtu dhidi ya jambo fulani. Kwa mfano, ” wewe, utakiona leo, nitakuchezesha unyago wa kima”. Inaaminika kuwa kima huacheza ngoma (Unyago) ili kuwatoa vigori (Wali). Tendo hili  hufantika kwa siri na endapo watagundua umewaona, lazma nawe uchezeshwe. Kwa hivyo, kuwa makini na mambo ya watu, usije ukachezeshwa unyago wa kima!
  1. Bura yangu sibadili na rehani
Huu ni msemo ambao una maana lukuki, baadhi ya watu hutafsiri neno “bura’ kama kitu cha tunu kichakavu. Kwa hivyo msemaji wa msemo huu hunamaanisha kuwa hawezi badili kitu chake cha tunu kwa kipya.
  1. Usiache “mbachao” kwa msala upitao
Katika msemo huu, wahenga wametumia neno “mbachao” linatamkwa “m-bachao,” yaani ni kifaa duni kinachotumiwa kufanyia ibada, Kwa mfano, mkeka au jamvi kuukuu (Kidukwa)..sasa wamesisitiza usije ukauacha kwa “Msala” upitao..msala nao ni sehemu ya kusalia lakini si duni kama ilivyo m-bachao. Pia, msemo huu un maana sawa na Usiyadharau madafu, maembe ni ya msimu.
  1. Mwanya ni kilema pendwa
 Wengi hawafahamu kuwa hata kama mwanya ni kilema, lakini ni kilema kinachopendwa na wengi. Vilema vya aina hii hutambulika kama ‘vilema pendwa’, vipo vingi kwa uchache ni baadhi ya matege ya miguu, makalio makubwa, vifua, na misuli mikubwa.
  1. Mungu hakupi kilema akakunyima mwendo
Msemu huu una maana kuwa mtu anapaswa kuridhika na alicho nacho. Funzo kuu ni kuwa haina haja kutamani vitu ambavyo vimepiku uwezo wetu.
  1. Mlevi haukubali ulevi
Msemo huu una maana kuwa hata anywe vipi hakubali kuitwa mlevi. Msemo hu umewalenga mahasidi na mafisadi ambao hukataa chungu ya ukweli.
  1. Chongo kwa mnyamwezi kwa mswahili amri ya mungu
Wengne hutumia neno ‘chogo’ badala ya ‘chongo’, yote kheri alimradi haipotosha maana ya usemi huu.
  1. Ushikwapo shikamana, si wengi wa kupendana
Maana ya msemo huu ni, endapo atatokea mtu akakupenda na akaomba muwe marafiki usikatae, kwani hapa ulimwenguni watu wachache sana wanaopendana.
  1. Maji! Ni kumbwe na kinyweo, matupu yasonga moyo
 Maana ya msemo huu ni kuwa, kunywa maji pekee bila ya kula chakula yaweza kusumbua tumbo. Ni vema upatapo mgeni umpe chakula kwanza halafu ndo umpe maji. Ni vizuri uelewe kuwa msemo huu unaweza kuwa na maana tofauti tofauti kulingana na muktadha uliotumika.
  1. Akomelepo mwenyeji na mgeni koma papo
 Msemo huu wa kiswahili una maana kwamba mgeni anapaswa fuatisha mipaka ya mwenyeji wake. Endapo atakushawish jambo fulani,usipinge.
  1. Pema usijapo pema, ukipema si pema tena
maana ya msemo huu ni kuwa, mahala popote huwa pazuri endapo hujawahi kwenda. Ukishaenda mara kwa mara uzuri wake huisha. Hutumika kuonya mtu dhidi ya kuzoea jambo fulani kwa uzuri wake kwa sababu anaweza kuzoea ule uziri na pindi ukipotea hatakuwa na sababu ya kulipenda jambo hilo.
  1. Mwanaharamu hata umtie kwenye chupa atatoa japo kidole ili ajulikane kama yupo
Msemo huu unamlenga mtu aliye na tabia mbaya. Maana yake ni kuwa, popote aendapo lazma atataka mtambue uwepo wake.
  1. Afugae ng’ombe tume, mwenye ziwa la kujaza
Usemi huu una maana kuwa, fanya kazi kwa bidii na utafaidi matunda ya kazi ya mikono yako. Msemo mwinigine ulio na maana sawa ni ‘mwenye kisu kikali ndiye ataekula nyama.’
  1. Usione ukadhani
Huu ni msemo ambao nafahamika na wengi. Una maana kuwa, usije liona jambo na ukaridhika na tafsiri ya awali. unapaswa ulichunguze kwa makini ili upate uthibitisho wake pengine lina maana tofauti. Msemo huu unatufunza umuhimu wa kuhakiki jambo fulani ili kuhepuka tafsiri hasi.
  1. Punda afe mzigo wa bwana ufike
Msemo huu hautushawishi kuua punda ili kufikisha mzingo. Una maanana kuwa, weka lengo la kutimiza wajibu wako. Labda kutakuwa na vizuizi katika kutimiza wajibu, lakini ili kulinda hadhi na cheo chako iwe kazini au popote pale ulipopewa wadhifa,jitahidi utimize wajibu wako kwa gharama yoyote.
  1. Usimlaumu mungu kwa kumuumba chui, mshukuru hakumpa mbawa
Maana kuu ya msemo huu ni kwamba, unapaswa kumshukuru mungu kwa hicho mungu alichokujaalia, wala usikosoe uumbaji wake. Funzo kuu kutokana na msemo huu ni kuwa mungu huumba au hutoa kwa makadirio maalum, hazidishi wala hapunguzi. Hebu fikiria kama chui andegukuwa na mabawa tungekuwa wapi.
  1. Maji ya kifuu bahari ya chungu
Msemo huu una maana kuwa jambo dogo unalolidharau wewe, wenzako linawatoa jasho. (maji ya nazi mdudu chungu/sisimizi kwake sawa na bahari).
  1. Mgala mwue na haki yake umpe
Maana  ya musemo huu ni kuwa, Hata kama umeamua kumkandamiza mtu kwa kumfanyisha kazi ngumu ama malipo duni, mtimizie ulichomwahidi ama iliyo haki yake.
  1. Kutoa ni moyo usambe ni utajiri
Msemo huu unatufunza kwamba kuwasaidia wengine si kuonyesha utajiri mtu alionao bali ni ishara ya upendo na kujali maslahi ya wengine.
  1. Bure huchosha
Msemo huu unadhamiria kutufunza kuwa si vizuri kuzoea kupenda kupokea vitu bila kufanya kazi. Tabia hii ya kupokea tu hukwaza wanaotupa, ama labda wao wakatusema vibaya na kutukera.
  1. Ampaye shetani maana,hujipatisha ghadhabu za Rahamani
Msemo huu unamaanisha kuwa anayemsifu shetani au mtu mwovu humchukiza Muumba na kujiletea adhabu. Msemo huu unatuonya kama wanajimii dhidi ya kuwapa watu waovu sifa nzuri.
  1. Bahati yenda kwa wawi wema wakalia ngoa
Maana ya msemo huu ni kuwa bahati ikiwaendea watu waovu, wema huwewaonea wivu iweje wamebahatika? Husistaajabishwe na hayo kwani bahati haibagui.
  1. Akuchukiaye hakosi hila ya kukutia
Maana ya msemo huu ni kuwa, mtu asiyekupenda anaweza kukuzushia mabaya ilimradi tu, akuchafue, akuharibie sifa zako, au mambo yako.
  1. Waja kufa na laiti na vyanda kinywani
Msemo huu unatufunza kuwa tusipozingatia ushauri ama makanyo tutaishia tukifikwa na mabaya na tujutie kutoyazingatia.
  1. Afichaye ugonjwa hufichuliwa na kilio
Funzo kuu katika msemo huu ni kuwa anayefanya siri matatizo yake huumbuka pale yanapomzidi ama kumgharimu hadi kuonekana.
  1. Utatumiaje mchuzi nyama usile
Msemo huu unawalenga watu ambao wnapenda kujinufaisha na mali ya watu wengine ilhali hawataki kuhusishwa na wao. Maana ya msemo huu ni iweje wamkataa mtu ilhali unajinufaisha na vilivyo vyake?
  1. Hutendwaje ikafana shubiri ikawa tamu?
Msemo huu unatufunza kuwa haiwezekani mtu kubadili jambo hata likawa kinyume na lillivyoumbwa au linavyofahamika.
  1. Midundo ikibadilika ngoma huchezwa vingine
Maana kuu ya msemo huu ni kuwa, mabadiliko yanapotokea katika mazingira yako, huna budi kubadili mbinu ili kukabiliana na mabadiliko hayo. Funzo kuu ni kuwa wanajamii wanapaswa kukubali mabadiliko badala ya kulalamika.
  1. Bata mtaga mayai usichinje kwa tamaa ya wingi
Msemo huu una funzo nzuri sana kwa wanajamii. Maana yake ni kuwa tamaa za haraka za kukifaidi kitu zisituponze tukaharibu manufaa makubwa zaidi ya kitu hicho hapo baadae.
  1. Samaki mkunje angali mbichi
Msemo huu ni muhimu sana katika jamii yetu. Unatufunza kwamba ni vinzuri kuwaonya watoto wetu tangu utotoni mwao ili kwafanya waelewe mambo na kujirekebisha kwa urahisi.
  1. Bahati ikibisha hodi sharti ufungue mlango mwenyewe
Msemo huu unamaanisha kuwa unapopata fursa ama nafasi ya kutenda jambo yakupasa uitumie vema na si kuipuuzia au kukata usaidiwe kuipokea. Kwa hivyo, ni vyema wanajamii wajifunze kutumia fursa tofauti tofauti kama inavyohitajika.
  1. Kipenda roho hula nyama mbichi
Msemo huu una maana kuwa, mtu hujitosa hata kuyatenda mambo yasiyo ya kawaida au magumu bora apate anachokipenda.
  1. Dunia tambara bovu ukivuta utachana
Msemo huu untuonya dhidi ya kuwaamini sana wanadamu. Maana yake ni kuwa, usiwaamini sana walimwengu au  kuwategemea sana kwani wanaweza kukutenda.
  1. Cha mchama huchama cha mgura hugura
Msemo huu una maana kuwa asiyekuwepo kulinda mali yake au kutunza mali yake huishia kutumiwa vibaya ama kumalizwa na wengine ambao labda hawana.
  1. Akopaye akilipa huondokana na lawama
Huu ni msemo ambao una funzo nzuri sana kwa wanajamii. Una maana kuwa anyekopa akilipa hujiondolea lawama. Kwa hivyo, ni wajibu wate kuhakikisha tumeiondolea lawama kwa kulipa madeni yote yanayotukabili.
  1. Achezaye na tope humrukia
Msemo huu una maana kuwa unaposhiriki kutenda uovu si ajabu mabaya hayo yakakudhuru mwenyewe. Kwa hivyo, msemo huu unatuonya dhidi ya kushiki katika kutenda uovu.
  1. Waarabu wa pemba hujuana kwa vilemba
Pemba ni mji fulani wa pwani na waswahili wanoishi huko huvalia vilemba. Msemo huu una maana kuwa watu a tabia moja hujuana kwa mambo wanyofanya.
  1. Lenye mwanzo lina mwisho
Msemo huu unamaanisha kuwa jambo lolote lililo na mwanzo lina mwiso. Msemo huu una maana sawa na hakuna ndefu lisilokuwa na mwiaso.
  1. Zunguo la mtukutu ni ufito
Msemo huu unatufunza kuwa njia ya kumfunza mtoto mkaidi ama asiyesikiliza ni kumpa adhabu.
  1. Maji usiyoyafika hujui kina chake
Msemo huu unamaanisha kwamba jambo ambalo hujalifanya hujui ugumu wake. Pia, msemo huu una maaana sawa na kitanda usichokilalia hujui kunguni wake.
  1. Ukiwaona ni watu moyoni hawana utu
Msemo huu unamaanisha kuwa usifikiri kwamba kila uliyekuwa karibu naye anakupenda kwa dhati wengine ndio maadui zako namba moja na ni vigumu kuwatambua.
  1. Afadhali jirani mbuge kuliko jirani mwenye mdomo mrefu
Msemo huu una maana kuwa mtu anayefitini wengine ni hatari kuliko hata mlafi.
Misemo ni muhimu sana katika jamii. Kwanza, ni njia ya kupitisha mafunzo kutoka kazazi kimaja hadi kingine. Pia, misemo huwafunza wanajamii kuhusu utamanduni wao, ni njia ya kujiburudisha na pia hutumika kuonya au kushauri.
Kwa hivyo, ni vyema wanajamii kuitumia misemo kila siku kwani itawajenga kielimu na pia kimaadili.

Deja un comentario

Tu dirección de correo electrónico no será publicada. Los campos obligatorios están marcados con *